Obama alaani mashambulizi ya Garissa


Marekani imelaani vikali mashambulizi ya Jumapili katika makanisa mawili huko Garissa, Kenya na kuuwa watu wapatao 17 huku wengine zaidi ya 40 wakiwa wamejeruhiwa.

Kwa mujibu wa VOA mashambulizi hayo ya Garissa yametokea siku chache kufuatia kuuawa kwa mfanyakazi mmoja wa misaada na kutekwa kwa wengine wanne kutoka kambi ya wakimbizi ya Daadab, na kabla ya hapo kulitokea shambulizi katika klabu moja ya starehe mjini Mombasa wiki iliyopita.

Taarifa ya White House iliyotolewa Washington Jumapili jioni ilisema watu waliofanya mashambulizi hayo hawakuonyesha heshima yoyote kwa maisha ya binadamu, na ni lazima wakamatwe na kufikishwa mbele ya sheria mapema iwezekanavyo.

About these ads

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out / Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out / Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out / Change )

Connecting to %s

Follow

Get every new post delivered to your Inbox.

Join 1,706 other followers