BOKO HARAM WAITOLEA VITISHO VOA

Kundi moja la wanamgambo limewatishia mashirika kadhaa ya kimataifa na ya nyumbani ikiwa ni pamoja na idhaa ya Hausa ya Sauti ya Amerika.
Kwa mujibu wa VOA vitisho hivyo viko kwenye video ya dakika 18 kwenye mtandao wa You tube Jumanne kwa jina la kundi la kiislam la Boko Haram.
Video hiyo inaonyesha gari ikilipuka mjini Abuja Alhamisi nje ya jengo la This Day moja ya gazeti mashuhuri la taifa.