Archive for September, 2011

Kiongozi wa Alqaeda Yemen Al awlaki auwawa katika operesheni Troy.

Posted in Uncategorized on September 30, 2011 by sunday Shomari

Kiongozi wa Alqaeda wa Ymen aliyekuwa akijificha katika milima ya nchi hiyo Anwar Al Awlaki ameuwawa na mashambulizi ya bomu ya vikosi vya Marekani.

Amekuwa ni Mmarekani wa kwanza kuuwawa kwa amri ya Whitehouse katika shambulizi kila mabomu lijulikanalo kama Operesheni Troy. Al Awlaki ni mzaliwa wa Marekani na amewahi kuwa Imam wa msikiti mmoja wa Alexandria Virginia.

Kwa mujibu wa jarida la Usa today Al awlaki alishiriki katika kupanaga mashambulizi kadhaa dhidi ya Marekani ikiwa ni pamoja na bomu lililoshindwa kulipuka lililofichwa kwenye nguo ya ndani na raia wa Nigeria Abdul Mutalab. Pia amehusishwa na Meja Haassan Nidal aliyefyatua risasi na kuuwa wanajeshi kwnye kambi ya jeshi huko Texas.

Serikali ya Obama kwa mara nyingine imeonyesha uwezo wake wa kupambana na ugaidi nje ya Marekani kwa staili ya kuwaondoa wakuu wa mitandao lakini safari hii kuna utata kutoka kwa wakosoagi wa serikali wakidai kwamba raia wa Marekani hawezi kuuwawa kwa staili hiyo bila kupata kwenda mahakamani.

Lakini serikali ya Obama imeshaeleza kuwa mtu huyo alikuwa kwenye orodha ya CIA ya maadui wanaotafutwa au kuuuwawa kwa sababu ni adui wa nchi. Baba yake Al awlaki kwa upande wake aliwahi kupinga uamuzi huo wa serikali mahakamani lakini alishindwa.

Huku ikiripotiwa helikopta kupotea Shamsi Vuai asema “Hatumchagui mfalme wa Igunga”.

Posted in Uncategorized on September 30, 2011 by sunday Shomari

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, helikopta inayotumiwa na CCM katika kampeni za Igunga imeripotiwa kupotea ikiwa angani wakati ikijaribu kutafuta vituo vilivyopangwa kwa ajili ya kumnadi mgombea ubunge wa chama hicho, Dk Dalaly Kafumu.Taarifa za kupotea kwa helikopta hiyo zilianza kuzagaa alhamisi majira ya saa tano asubuhi mjini Igunga na baadaye zilithibitishwa na mmoja wa maofisa wa CCM ambaye hakutaka jina lake litajwe kuwa walipotea mara kadhaa baada ya mtu wanayemtegemea kuwaongoza njia kupoteza ramani akiwa angani.

“Unajua tumemchukua mtu ambaye anaifahamu vizuri Igunga ili aweze kuielekeza helikopta mahala pa kwenda, lakini kwa bahati mbaya mtu huyo alipokuwa angani alishindwa kwa sababu ya kupoteza ramani,” alisema ofisa huyo.

Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi taarifa za awali za kupotea kwa helikopta hiyo zilitolewa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe katika mkutano wa kampeni wa chama hicho uliofanyika katika Kata ya Nkinga jana asubuhi, akisema kuwa alipata habari kuwa helikopta ya CCM ilikuwa imepotea.Mmoja wa watu waliokuwa ndani ya helikopta hiyo alisema walipotea mara kadhaa na kwamba katika harakati hizo walitua kwenye kijiji kimojawapo cha Wilaya ya Igunga jana saa nne asubuhi, lakini walijikuta kwamba wamekosea, hivyo kuondoka kwani watu hawakuwa tayari kwa mkutano huo.Kusoma zaidi bofya Read more »

Rais Chavez alaumu vyombo vya habari

Posted in Uncategorized on September 30, 2011 by sunday Shomari

Rais wa Venezeulela Hugo Chavez ameenda kwenye televisheni kufuta uvumi juu ya Afya yake, siku moja baada ya gazeti moja kuripoti kuwa alikimbizwa hospitali kwa matatizo ya figo ikihusishwa na matibabu ya kansa yake.

Kwa mujibu wa VOA Bw. Chavez Alhamisi alionekana kwenye televisheni akiwa amevaa kofia na fulana nyekundu akirusha mpira kwenye viwanja vya kwenye viwanja vya jumba la rais vya Miraflores huko Caracas.

Kiongozi huyo wa Venezuela pia alikosoa vyombo vya habari kwa kuuliza mno juu ya hali yake. Rais Chavez hajasema ni kansa gani aliyonayo.

Bingu wa Mutharika amfutia marufuku rais mpya wa Zambia!

Posted in Uncategorized on September 30, 2011 by sunday Shomari

Rais wa Malawi Bingu wa Mutharika amesema serikali yake itamruhusu rais mpya mteule wa nchi jirani ya Zambia kuingia Malawi baada ya kufukuzwa nchini humo miaka minne iliyopita.

Kwa mujibu wa VOA serikali ya bwana Mutharika ilisema alhamisi kwamba rais Michael Satta aliyechaguliwa kuwa rais wa Zambia wiki iliyopita ameondolewa marufuku ya masuala ya uhamiaji, kwa sababu sasa ni mkuu wa nchi.

Mwaka 2007 maafisa wa Malawi walimkamata bwana Satta alipokuwa katika safari binafsi kwenye mji wa kibiashara wa Blantyre. Maafisa wa usalama walisafiri naye maili kadhaa kwenda kwenye mpaka wa Zambia kabla ya kumshusha na kumpa hati ya kupigwa marufuku kuingia nchi hiyo.

DSK uso kwa uso na adui yake wa Ufaransa!

Posted in Uncategorized on September 30, 2011 by sunday Shomari

Mkuu wa zamani wa shirika la fedha duniani IMF Dominique Strauss Khan alifanya mkutano wa saa mbili na mwandishi wa Ufaransa Tristane Banon ambaye alimshutumu kwa kutaka kumbaka baada ya kumpeleka kwenye nyumba isiyo na watu kwa ahadi ya kufanya mahojiano.

Kwa mujibu wa VOA mkutano huo wa uso kwa uso ulifanyika bila wanasheria kuwepo katika kituo cha Polisi cha Paris jana. Wapelelezi wa Polisi walikuwepo na mkutano huo utaweza kuamua kama waendesha mashitaka watafungua mashitaka kwenye kesi hiyo.

Hakuna upande uliobadili dai lake kwenye mkutano huo. Strauss Kahn ameyaita madai hayo kuwa ya kufikirika na kusema mkutano wao ulikuwa wa makubaliano ya pande zote mbili. Banon anasema Strauss Kahn alijaribu kumlazimisha na hivyo akachana nguo zake wakati akijaribu kumzuia.

Moto wa Afrika kaskazini unataka kuhamia Cameroon?

Posted in Uncategorized on September 30, 2011 by sunday Shomari

Maafisa wa usalama na mashahidi wanasema watu waliokuwa wamevalia sare za kijeshi na kubeba mabango yanayompinga rais wa muda mrefu wa Cameroon Paul Biya wamefyatua risasi katika daraja moja kubwa katika mji mkubwa wa nchi hiyo, Douala.

Kwa mujibu wa VOA mashahidi wanasema kwamba watu waliokuwa na silaha waliweka vizuizi kwenye daraja la Wouri lenye safari nyingi , na kufyatuliana risasi na vikosi vya usalama kwa saa kadhaa mapema Alhamisi. Haikufahamika haraka ni watu wangapi waliokuwa na silaha waliohusika. Pia kuna ripoti kwamba vikosi vya usalama viliwakamata watuhumiwa wanne na kwamba mtuhumiwa mwingine alitorokea chini ya daraja kuelekea kwenye mto.

Ajali mbaya barabara ya Iringa Mbeya

Posted in Uncategorized on September 30, 2011 by sunday Shomari

Na Francs Godwin Iringa,

Habari iliyoufikia mtandao huu kutoka kijiji cha Ifunda wilaya ya Iringa vijijini katika barabara kuu ya Iringa-Mbeya zinadai kuwa mtu mmoja amekufa papo hapo baada ya usafiri wa power tilla ambayo alikuwa akisafiri nayo kugongana na gari kubwa na kusababisha kifo chake.

Mashuhuda wa tukio hilo wamedai kuwa ajali hiyo imetokea muda wa saa 2 usiku wakati dereva wa Power Tilla hiyo Nico Mhengilolo mkazi wa Kilimahewa alipokutwa na mauti .Kusoma zaidi bofya Read more »

Ibada ya Kiswahili-Columbus Ohio

Posted in Uncategorized on September 29, 2011 by sunday Shomari

Usiku wa King Kiki

Posted in Uncategorized on September 29, 2011 by sunday Shomari

King Kiki Night

Posted in Uncategorized on September 29, 2011 by sunday Shomari

Follow

Get every new post delivered to your Inbox.

Join 1,705 other followers