Archive for June, 2011

Happy Birthday Congo miaka 51

Posted in Uncategorized on June 30, 2011 by sunday Shomari

Na Austere Malivika.

Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imesheherekea sikukuu ya uhuru ikiwa hivi sasa ni miaka 51 tangu nchi hiyo ijikwamue kutoka ukoloni.

Japokuwa wananchi wametoka katika ukoloni huo lakini hali ya wananchi wakawaida haijaboreka bado.

Sherehe za Alhamisi zilifanyika mjini Lubumbashi jimboni Katanga zikihudhuriwa na Rais Joseph Kabila.

Na huko mashariki mwa nchi hiyo hasa mjini Goma kulikuwa na gwaride kubwa la kijeshi kuadhimisha sherehe hizo.

Maandamano ya kuunga mkono Watanzania Uk.

Posted in Uncategorized on June 30, 2011 by sunday Shomari


Waandamaji Majuu wakipinga uhuni waliofanyiwa Watanzania kutoka kwa BAE Systems- picha kwa hisani ya Haki Ngowi Blogspot.com

NATO kuendeleza majamboz Libya

Posted in Uncategorized on June 28, 2011 by sunday Shomari

Kamanda wa NATO wa operesheni ya Libya anasema majeshi ya muungano hayapunguzi mashambulizi ya anga licha ya wito wa baadhi ya mataifa kusimamisha operesheni hiyo.

Luteni Jenerali wa Canada Charles Bouchard amesema operesheni hiyo inayoingia mwezi wa nne imepata maendeleo makubwa na kwamba mashambulizi dhidi ya raia na serikali ya Libya yamepungua.

Kwa mujibu wa VOA maelezo ya NATO yamekuja wakati mwendesha mashitaka wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu akiwataka wasaidizi wa Moammar Gadhafi wamkamate na wamfikishe kwenye mahakama hiyo kujibu kesi.

Soma zaidi bofya Read more »

Mr.Tz na Jr. waja na remix ya Careless Whispers

Posted in Uncategorized on June 28, 2011 by sunday Shomari

Rapper Chipukizi wa Washington Dc Jumbe Hamza a.k.a Mr. Tz akiwa na Jr. na kitu hicho Careless Whispers kusikiliza bofya hapo chini.


Mahakama ya kimataifa ya uhalifu yatoa hati ya kukamatwa Gadhafi

Posted in Uncategorized on June 27, 2011 by sunday Shomari

Majaji katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC wametoa hati ya kukamatwa kwa kiongozi wa Libya Moammar Gadhafi na wasaidizi wake wawili waaminifu.

Uamuzi huo umekuja baada ya mwendesha mashitaka wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu Luis Moreno Ocampo kuomba hati hizo zitolewe dhidi ya Gadhafi na mtoto wake Seif al Islam na mkuu wa shirika la ujasusi Abdullah al Senussi. Kwa habari zaidi bofya hapa.

Read more »

Mambo ya Carnival Dc

Posted in Uncategorized on June 26, 2011 by sunday Shomari


Hii tu ni sehemu ya mambo yalivyokuwa kwenye Carnival mjini Washington Dc jumamosi .(Picha kwa hisani ya Swahili Villa blogspot.com)

Habari ndio hiyo “Ultra white Cruise party”.

Posted in Uncategorized on June 26, 2011 by sunday Shomari



Hii ndio sehemu tu ya ndani ya boti ya maakuli katika Ultra White Cruise Party itakayofanyika July 2. Mambo yatakuwa mswano kazi kwenu watu wa DMV “asiye na mwana ataeleka jiwe”.

Wabunge wa Tanzania wanaofuatilia malipo wanena huko London

Posted in Uncategorized on June 26, 2011 by sunday Shomari

Mexico yatwaa kombe la CONCACAF GOLD CUP

Posted in Uncategorized on June 26, 2011 by sunday Shomari

Timu ya taifa ya Mexico.

Timu ya taifa ya Mexico jumamosi ilithibitisha kutangulia si kufika baada ya kutoka nyuma wakiwa wamepigwa bao 2-0 na hatimaye kurudisha yote na kushinda kwa jumla ya mabao 4-2 dhidi ya timu ya taifa ya Marekani.

Mechi hiyo ikiangaliwana watazamaji zaidi ya 90,0000 ilianza taratibu huku kila mmoja akimsoma mwenzake na ndipo Marekani walipopata bao 2 za haraka haraka.

Baada ya Landon Donovan kupachika la pili Mexico walikuja juu na kusawazisha mabao hayo ambayo yalidumu mpaka mapumziko.

Kipindi cha pili kilianza kwa Mexico kucheza kwa kasi na kupachika bao la tatu na hatimaye walipachika msumari wa mwisho kwenye jeneza la Marekani kwa kufunga goli la nne baada ya kipa mkongwe Tim Howard kutoka golini kujaribu kuokoa hatari golini mwake kutoka kwa mshambuiaji hatari wa Mexico Giovanni Dos Santosh aliyepachika bao la nne.

Mpaka mwisho wa mchezo Mexico 4 na Marekani 2. Hivyo Mexico ndio mabingwa wa CONCACAF 2011 naye Javier Hernandez alikuwa mfungaji bora wa michuano kwa kupachika mabao 7. Wakati mchezji bora wa mechi hiyo alikuwa Giovanni Dos Santosh.

Leo ni kumbukumbu ya MJ

Posted in Uncategorized on June 25, 2011 by sunday Shomari


Ni miaka miwili tangu mfalme wa pop duniani Michael Jackson alipoaga dunia Juni 25,2009. Duniani kote Michael Jackson anakumbukwa .

Na kwa mujibu wa Nielsen Sound Scan mauzo ya nyimbo zake yameendelea kwenda juu hapa Marekani, tangu kufariki kwa Michael mpaka kufikia Juni 2011 zilikuwa zimeshauzwa milioni 16.3 na albam zake nakala milioni 10.6.

Mauzo ya album za MJ baada ya kifo chake yanakadiria kuwa asilimia 33 ya mauzo yake yote yamepatikana baada ya kifo chake.

Follow

Get every new post delivered to your Inbox.

Join 1,705 other followers