Kila la kheri mwakilishi wa Tanzania kwenye Miss Universe!
Hellen Dausen mwakilishi wa Tanzania katika shindalo la 59 la Miss Universe hapa Marekani atapeperusha bendera ya Tanzania kwenye shindano hilo ambalo litaonyeshwa moja kwa moja na Televisheni ya NBC Agosti 23,2010 hapa Marekani.
Washiriki wa shindano hilo hivi sasa tayari wameanza kupewa alama zao za juu zikiwa kwa wale wanaoonekana kuwa na uwezo wa kufanya vyema kwenye shindano hilo litakalofanyika huko Mandalay Bay Las Vegas.
Hivi sasa nyota zimeanza kuonekana miongoni mwa washiriki ambapo alama za juu mpaka wakati huu zinashikiliwa na Mwakilishi wa Phillipines Venus Raj akiwa na pointi 3.74 naye mwakilishi wa Afrika mwenye alama za juu kidogo ni mwakilishi wa Ghana Awurama Simpson akiwa na pointi 2.53 naye mwakilishi wa Tanzania Hellen Dausen anazo pointi 1.95. Mashindano haya yanashirikisha wananchi kutoka nchi 83 duniani. Kila la kheri Hellen Dausen.

